Home » Tanzania » (ICC) ishughulikie manung’uniko ya kuwawajibisha viongozi wa Afrika pekee

(ICC) ishughulikie manung’uniko ya kuwawajibisha viongozi wa Afrika pekee

09 February 2016 | Tanzania

Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita  (ICC) imetakiwa kushughulikia manung’uniko yanayohusu kuwawajibisha viongozi wa Afrika pekee ili kukifanya chombo hicho kiendelee kutoa haki na kuheshimika

Akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na mahakama hiyo katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa jijini Arusha nchini Tanzania, Waziri wa Katiba na Sheria  nchini Tanzania Dr.Harisson Mwakyembe  ameitaka mahakama hiyo kufanyia kazi manung`uniko ya bara la Afrika licha ya Tanzania kuunga mkono shughuli za mahakama hiyo lakini bado iko kwenye msimamo wa nchi hizo.

Tayari viongozi wa umoja wa Afrika katika mkutano wao wa  mjini Addis Ababa hivi karibnuni walitoa pendekezo la kujitoa katika mahakama ya ICC yenye makao yake makuu  The Heague nchini uholanzi
Mahakama ya Kimataifa ya  makosa ya jinai ICC inaendelea na semina ya siku tano kwa wanasheria wa ndani na nje ya bara Afrika  wameikuhusu namna ya  kutumia mahakama hiyo kutetea haki za binadamu na utawala bora.

Ad