Home » Tanzania » Uteuzi wa wenyeviti wawili wa hifadhi za jamii na Mmoja wa Chuo

Uteuzi wa wenyeviti wawili wa hifadhi za jamii na Mmoja wa Chuo

21 November 2016 | Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa wenyeviti wawili wa bodi za mashirika ya hifadhi za jamii na mmoja wa chuo.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imewataja walioteuliwa kuwa ni kama ifuatavyo;

Kwanza, Rais Magufuli amemteua Mhandisi Alhaji Mussa Iyombe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF).

Mhandisi Alhaji Mussa Iyombe ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Pili, Rais Magufuli amemteua Prof. Faustine Karani Bee kuwa Mwenyekiti wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF)

Prof. Faustine Karani Bee ni Makamu Mkuu wa Chuo cha Ushirika Moshi.

Tatu, Rais Magufuli amemteua Prof. Tadeo Andrew Satta kuwa Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).

Kabla ya uteuzi huu Prof. Tadeo Andrew Satta alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

 

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

19 Novemba, 2016

Ad