Home » Tanzania » Rais Magufuli ateua kamati maalum ya pili ya wachumi na wanasheria kuchunguza mchanga wa madini

Rais Magufuli ateua kamati maalum ya pili ya wachumi na wanasheria kuchunguza mchanga wa madini

10 April 2017 | Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 10 Aprili, 2017 ameteua wajumbe wa kamati maalum ya pili itakayofanya uchunguzi wa madini yaliyomo kwenye mchanga wenye madini ulio ndani ya makontena yaliyopo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kamati hiyo inajumuisha wachumi na wanasheria na imetanguliwa na kamati ya kwanza iliyoundwa na wataalamu wa masuala ya jiolojia, kemikali na uchambuzi wa kisayansi.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imewataja wajumbe wa kamati hiyo kuwa ni;

  1. Prof. Nehemiah Eliachim Osoro
  2. Prof. Longinus Kyaruzi Rutasitara
  3. Dkt. Oswald Joseph Mashindano
  4. Bw. Gabriel Pascal Malata
  5. Bw. Casmir Sumba Kyuki
  6. Bi. Butamo Kasuka Philip
  7. Bw. Usaje Benard Usubisye
  8. Bw. Andrew Wilson Massawe

Wajumbe hao wataapishwa na Mhe. Rais Magufuli kesho tarehe 11 Aprili, 2017 saa 3:00 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.

 

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

10 Aprili, 2017

 

Ad