Home » Tanzania » Rais Magufuli afanya uteuzi wa Kaimu Jaji Mkuu wa Mahakama Tanzania

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Kaimu Jaji Mkuu wa Mahakama Tanzania

18 January 2017 | Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, tarehe 17 Januari, 2017 amemteua Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Juma kuwa Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania.

Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Juma anachukua nafasi ya Mhe. Jaji Mohamed Chande Othman ambaye amestaafu.

Kabla ya kuteuliwa kushika nafasi ya Kaimu Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Juma alikuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania.

Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Juma atakaimu nafasi ya Jaji Mkuu wa Tanzania mpaka hapo Mhe. Rais Magufuli atakapofanya uteuzi wa Jaji Mkuu wa Tanzania.
Uteuzi wa Mhe. Jaji Prof. Ibrahim Juma unaanza mara moja.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
17 Januari, 2017

Ad