Home » Tanzania » Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

10 October 2016 | Tanzania

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemteua Mhandisi James Mitayakingi Kilaba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Mhandisi James Mitayakingi Kilaba umeanza jana Jumamosi tarehe 08 Oktoba, 2016.

Kabla ya uteuzi huo, Mhandisi James Mitayakingi Kilaba alikuwa akikaimu nafasi hiyo, baada ya uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Ally Yahaya Simba kutenguliwa.

 

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

09 Oktoba, 2016 

Ad