Home » Nje ya Afrika

Nje ya Afrika

24 May 2016
Waziri Mkuu wa Ufaransa Manuel Valls amekutana hapo jana na mwenzake wa Israel Benjamin Netanyahu jijini Yerusalemu kuzungumzia mapendekezo ya kuwepo kwa mkutano wa kimataifa kufufua juhudi za amani na Wapalestina. Hata hivyo, Netanyahu, ametupilia mbali mapendekezo hayo na badala yake kuomba pawepo na mazungumzo ya ana kwa ana baina yake na Rais... [Read More]
12 May 2016
Bunge la Seneti Brazil limepiga kura kuamua kuidhinisha kura ya kutokuwa na imani dhidi ya kiongozi wa taifa hilo Dilma Rousseff. Atasimamishwa kazi ya urais kwa siku zisizozidi 180 wakati bunge hilo la Seneti litakagua tuhuma zinazomkabili. Bi Rousseff anatuhumiwa kubadili kinyume cha sheria fedha za serikali kuficha nakisi inayoongezeka ya umma... [Read More]
20 April 2016
Rais wa Marekani Barack Obama amewasili nchini Saudi Arabia kwa ziara ya siku mbili. Obama anatarajiwa kutumia ziara hii kuonesha ushirikiano wa nchi hiyo katika vita dhidi ya Wanajihadi. Mzozo wa Syria na Yemen pia utajadiliwa katika ziara hiyo. Baadhi ya wanasiasa nchini Marekani walishtumu ziara hii ya rais Obama wakiishtumu serikali ya Riyadh... [Read More]
19 April 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Waziri Mkuu wa Japan Mheshimiwa Shinzo Abe kufuatia vifo vya watu zaidi ya 40 vilivyosababishwa na tetemeko la ardhi lililokikumba kisiwa cha Kyushu kilichopo kusini magharibi mwa nchi hiyo. Tetemeko hilo la ardhi limetokea Alhamisi iliyopita tarehe 14... [Read More]
19 April 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemuapisha Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe kuwa Balozi wa Tanzania nchini Japan. Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe ameapishwa leo tarehe 19 Aprili, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam. Mheshimiwa Mathias Meinrad Chikawe anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Batilda Salha Burian... [Read More]
14 March 2016
Polisi nchini Brazil, inasema kuwa zaidi ya raia milioni 3 wameandamana nchi nzima hapo jana, ikiwa ni maandamano makubwa kuwahi kushuhudiwa nchini humo, wakishinikiza kuondolewa madarakani kwa rais Dilma Rousseff. Wakiwa wamevalia mavazi ya rangi za njano na kijani kama zilizoko kwenye bendera ya nchi hiyo, wananchi hao wanalenga kuweka... [Read More]
14 March 2016
Chama cha kansela wa Ujerumani, Angela Merkel kimepata pigo kubwa kwenye uchaguzi wa majimbo uliofanyika hapo jana, ambapo wachambuzi wa mambo wanasema hali hiyo imetokana na sera ya chama chake kuhusu wahamiaji na wakimbizi. Chama cha mrengo wa kulia cha AFD kimeshuhudiwa kikiweka historia kwenye uchaguzi wa safari hii, baada ya kupata kura... [Read More]
14 March 2016
Rais wa Marekani, Barack Obama, ambaye juma lijalo atafanya ziara ya kihistoria nchini Cuba, amewahakikisha raia wa nchi hiyo wanaoishi ughaibuni, kuwa atatumia ziara hiyo kujadili masuala ya haki za binadamu na utawala wa Havana. Kwenye barua iliyocahpishwa mwishoni mwa juma kwa wanaharakati wanawake wa Cuba wanaoishi nchini Marekani, rais Obama... [Read More]
09 March 2016
Gavana wa zamani wa mkoa wa Katanga, Moise Katumbi amesema kuwa hakufurahishwa na kitendo cha polisi cha kuvamia Kanisa la Basilica St Mary jana mjini Lubumbashi, wakati alikuwa akishiriki ibada iliyoandaliwa katka muktadha wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake. Katumbi alijumuika na wanawake wanachama wa vyama vya upinzani katika... [Read More]
09 March 2016
Jeshi la Marekani imeeleza kuwa Kiongozi wa kundi linalojiita Islamic State Omar al-Shishani, maarufu kama Omar le Tchetchen ameuawa katika mashambulizi ya anga yaliotekelezwa mwishoni mwa juma lililopita. Taarifa hiyo ya jeshi la Marekani inasema huenda kiongozi huyo ameuawa na wapiganaji wemngine 12 wa kundi hilo katika mashambulio ya anga... [Read More]

Pages

Ad
Subscribe to Nje ya Afrika