Home » Bunge » Wabunge kujadili hotuba ya rais kwa siku tatu

Wabunge kujadili hotuba ya rais kwa siku tatu

26 January 2016 | Bunge

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya Bunge ni kwamba Kanuni ya 23 (1) (i) ya Kanuni za Bunge, toleo la Januari, 2016, Bunge litajadili Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyoitoa wakati wa ufunguzi rasmi wa Bunge jipya la Kumi na moja tarehe 20 Novemba, 2015 .

Mjadala kuhusu hotuba ya Mheshimiwa Rais unatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 26 hadi 28 Januari, 2016.

Hata hivyo ili kutoa nafasi kwa kila mbunge kuweza kuchangia bunge linatarajia kutengua kanuni na kuweka muda wa dakika 10 badala ya 15 za hapo awali kwa mbunge mmoja ili kutoa fursa kwa wabunge kuweza kujadili na kila mmoja apate nafasi,pia bunge liwe linaanza saa 10 jioni badala ya saa 11.

Ad