Home » Afrika » Mfanyabiashara mashuhuri nchini Kenya Jacob Juma, ameuwawa

Mfanyabiashara mashuhuri nchini Kenya Jacob Juma, ameuwawa

06 May 2016 | Afrika

Mfanyabiashara mashuhuri nchini Kenya Jacob Juma, ambaye amekuwa akizua mjadala mitandaoni kutokana na ujumbe wake anaoandika hasa kwenye Twitter, ameuawa kwa kupigwa risasi jijini Nairobi.

Taarifa zinasema Juma alipigwa risasi na watu ambao walikuwa wakiendesha pikipiki alipokuwa akielekea nyumbani kwake mtaa wa Karen majira ya saa nne usiku hapo jana.

Gari lake limepatikana na zaidi ya matundu 10 ya risasi huku polisi wakisema hakuna kilichoibiwa kutoka kwenye gari lake na simu zake mbili na pesa vilipatikana ndani ya gari.

Ad